Monday, June 17, 2013

LADY JAYDEE ALIVYOFUNIKA MWISHONI MWA WIKI, AKITIMIZA MIAKA 13 KATIKA FANI


Na Mahmoud Zubeiry, ONYESHO la mwanamuziki Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ kutimiza miaka 13 katika muziki, limefana usiku wa kuamkia Jumamosi katika eneo la maegesho ya magari kwenye ukumbi wa Nyumbani, Lounge, eneo la Kinondoni, Dar es Salaam kwa mamia kujitokeza kiasi cha kujaza eneo hilo, hadi kupishana ikawa taabu. Watoto wa mjini wanasema ilikuwa funika bovu- ndiyo shoo hiyo ilikuwa nzuri mno, ya kistaarabu, yenye mashamsham ya aina yake. 
Jide akikumbatiana na Profesa Jay


Jay akipagawisha


Jay akisema na nyomi


Mzee Kitime akimpiga picha Komando Kalala wakati anaimba 


Komando Kalala na mkewe jukwaani


Msanii Mango Star na nyoka


Mango Star na nyoka

Wasanii nguli wa Hip hop waliomsindikiza Jadyee katika shoo hiyo, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Joseph Haule na Juma Nature na kundi lake wanaume Halisi nao walifanya mambo mazuri jukwaani kiasi cha kuiongezea utamu shoo hiyo. Kufika saa 3:00 usiku tayari Machozi Band inayomilikiwa na Jide ilikuwa jukwaani kuanza kutumbuiza kabla ya kumpisha rapa Wakazi kutoka Ukonga, baadaye bendi ya M ikiongozwa na Grace Matata kwa shoo za utangulizi. Saa 5:00 usiku, Jide akapanda jukwaani na kuibua shangwe nzito kutoka kwa mamia waliokuwa wamefurika katika eneo hilo. Jaydee alianza na wimbo wa Nilishakuwaga na Wangu, baadaye akaimba Nakuhitaji, Moto, Mambo Bado, Yeye, Malaika, Siri Yangu, Wanock Nok kisha kumalizia na Single Boy katika awamu ya kwanza. Baada ya hapo, Jide akasema ilipotimu Saa 6:00 usiku ameingia katika mwaka mpya tangu azaliwe hivyo mashabiki wakamuimbia ‘Happy Birth Day’ kisha akateremka kwenda kukumbatiana na mama yake mzazi, Martha Mbibo na kumpa zawadi ya fedha zote alizokuwa ametuzwa jukwaani. Jide alirejea jukwaani na kuimba kwa ufupi nyimbo alizowahi kurekodi na wasanii Man Ngwair na Langa Kileo ambao hivi sasa ni marehemu, kabla ya kumpisha Mh. Mbunge wa Mbeya Mjini, Sugu ambaye aliimba nyimbo tatu tu, lakini alisisimua mashabiki ile mbaya. Sugu alianza na Hakuna Matata akimshirikisha Mkoloni, Sugu na kumalizia na Mambo ya Fedha ambao ulimrejesha jukwaani Jide. Kutoka hapo, ikawadia zamu ya Wanaume Halisi kutoka Temeke, wakiongoza na Juma Kassim Kiroboto ‘Sir Nature’, ambao nao walifanya balaa vile vile na kuurusha umati ile mbaya.
Msanii M2 The P akizungumza jukwaani
 
KR Mulla


Sir Nature


Nature na Doro
Sinta akimpiga picha Nature
Wakati Nature anaimba, mpenzi wake wa zamani Christine Manongi ‘Sinta’ alikuwa bize kumpiga picha ‘mzee’ wake wa kitambo, kiasi cha mmoja wa viongozi wa kundi hilo, Kiboya kupora kipaza sauti na kutamka Baba Sinta akimtania Nature, jambo ambalo liliwafanya watu washangilie.    Nature kabla ya kuanza kuimba alimpandisha jukwaani msanii M 2 P aliyezushiwa kifo wakati akiwa amelazwa Afrika Kusini sambamba na Man Ngwair. MP alisalimia na kushukuru kwa dua za Watanzania wakati akiwa taabani wadini, kwani zimemponya na akatumia fursa hiyo kumuombea swahiba wake Ngwair apumzishwe kwa amani peponi. Ndipo Wanaume wakaanza vitu vyao, wakipiga nyimbo za Sonia, Hakuna Kulala, Mzee wa Busara, Ladhia, Haipotei, Dance With Me na Jimwage. 
Jaydee na mama yake



Jaydee akikusanya fedha alizotuzwa


Anaziweka kwenye boksi kabla ya kweneda kumpa mama yake. Alyeshika boksi ni King Kiboya


TK wa M Band...


Maeneo kama haya Mh Sugu huwa si mkali...anajua kutabasamu


Rapa kutoka Ukonga


Alikuwepo...Mgaya Kingoba Mhariri wa Michezo gazeti la Habari Leo


Kutoka kulia Baraka Msilwa, Francis Kifukwe na mkewe

Wanaume walipoondoka akaibuka msanii mcheza ngoma za asili huku akichezea nyoka, Mango Star ambaye aliwaacha watu midomo wazi pale alipokuwa akimnyonya nyoka upande wa kichwani. Akafuatia mkongwe Komando Hamza Kelele ambaye kwanza alimpandisha mkewe, Stella John Momose Cheyo jukwaani kumtambulisha, kisha akaimba nyimbo na Tumetulia. Ikawadia zamu ya Profesa Jay, ambaye aliimba Joto Hasira pamoja la Lady Jaydee, baadaye, Teja, Yahya na Joto tena. Jaydee akateremka na kumuacha Jay amalizie shoo naye akamalizia vizuri kwa nyimbo za Hapo Vipi, Nikusaidiaje na Kamili Gado. Watu kadhaa waliofika Nyumbani Lounge kushuhudia shoo hiyo walilazimia kugeuka na kuondoka kwa sababu ukumbi ulikuwa ‘umejaa na hakuna pa kukanyaga’. Kwa ujumla shoo hiyo ilipendeza, ilikuwa bab kubwa. 
Credit to Bin zubery

CHADEMA YABWAGWA VIBAYA KATA ZA IRINGA



AHADI iliyotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu kwa katibu mkuu wa chama hicho Taifa, Abdulaman Kinana  kwamba watakibwaga Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mdogo wa madiwani mkoani hapa, imekuwa kweli.

Msambatavangu alimueleza Kinana alipopita hivi karibuni mjini Iringa wakati akielekea mkoani Njombe kwa ziara ya kikazi kwamba CCM itapata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi huo katika kata ya Ng’ang’ange  wilayani Kilolo na Mbalamaziwa, wilayani Mufindi.

“Niliahidi na imekuwa kweli kwasababu kazi ya maendeleo inayofanywa na serikali ya CCM inazidi kurejesha imani kwa wananchi na inadhihirisha jinsi wanavyopuuza kelele za baadhi ya wanasiasa wanaopinga maendeleo yanayofanywa,” alisema

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katika kata ya Ng'ang'ange, msimamizi msaidizi  wa uchaguzi huo, Esabela  Kamwela alisema jumla ya  wapiga kura  919 kati ya  1087 waliojiandikisha walishiriki uchaguzi huo.

Alisema Chadema ilimsimamisha Lucas Chahe huku CCM ikimsimamisha Nangamleki Yohanes katika  uchaguzi huo uliomaliza katika hali ya utulivu na amani.
Kamwela  alisema katika  uchaguzi huo kura 16 ziliharibika  huku mgombea wa Chadema akianguka  vibaya kwa  kupata  kura 217 na mgombea wa CCM akiibuka  kidedea kwa kuzoa kura 686.

Katika kata ya Mbalamaziwa ambako Chadema ilijipata matumaini ya ushindi kwa kile kilichoonekana mikutano yake kupata idadi kubwa ya watu, mgombea wake alibwagwa vibaya dhidi ya mgombea wa CCM.

Katika kata ya Mbalamaziwa ambako ni jirani kabisa na kata  ya Nyololo ambayo imeingia katika vitabu vya historia baada Septemba 2, mwaka jana wananchi wake kuhuhudia tukio ambalo halikuwahi kutokea katika nchi hii la mwandishi wa habari Daudi Mwangosi kuuawa wakati Chadema ikiendelea na harakati zake za kuimarisha chama chao,  mgombea  wake  Ezekiel Mlyuka aliambulia kura 185 tu kati ya kura 1,611 zilizopigwa.

Mgombea wa CCM, Zuberi Nyomolelo aliibuka mshindi wa kiti hicho cha udiwani baada ya kupata kura 1,426; kura  26 zikiharibika .

Katika mazingira ya kufurahisha, wagombea wa vyama vyote wameyakubali matokeo hayo, huku wafuasi wa CCM na wateule wao wakiendelea na shamrashamra wakisubiri siku ya kuapishwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.

Tuesday, June 11, 2013